Washa tochi/kamera ya kwenye simu janja kwa kuitikisa simu tuu


Washa tochi/kamera ya kwenye simu janja kwa kuitikisa tuu

Simu janja zimekuwa msaada kwetu kwa mambo mengi ambayo zimekuwa zikirahisisha shughuli kadha wa kadha kwenye ulimwengu huu wa teknolojia. Ile taa ya kuongeza mwangaza pembeni ya kamera ya nyuma ni tochi pia ambayo unaweza kuiwasha kiurahisi kabis

Uwepo wa taa pembeni ya

 kamera imekuwa na kazi zaidi ya moja 

na wale ambao tunapenda 

kuongeza ubora wa picha kabla 

ya kupiga ama inatokea upo

 sehemu yenye mwanga hafifu na

 unahitaji msaada wa kuona kitu 

fulani vizuri hakika tunashukuru kwa

 simu janja zetu kuwa na kitu

 ambacho kimewekwa kwa ajili 

ya kazi hiyo.

Sasa inatokea wakati fulani unatamani upate wepesi wa kuwasha/kuzima tochi au kamera bila ya kufuata hatua ambazo sote tunazifahamu lakini inakuwa haiwezekani. Changamoto inapotokea ndio inakuwa chachu ya kutafuta jibu la kitu fulani na kutokana na ukuaji wa teknolojia suala zima la kuwasha ama kuzima iwe tochi au kamera ni rahisi kabisa.


Fahamu kuhusu Shake Flashlight & Camera

Shake Flashlight & Camera ni programu tumishi inayopatikana kwenye Playstore ikiwa imetengenzwa kumwezesha mwenye simu janja ya Android kuwasha/kuzima tochi au kamera kwa kuitikisha tu kwa mara kadhaa. FUata hatua hizi ili uwe unaweza kuwasha na kuzima kamera/tochi kwa urahisi sana:

>Mara baada ya kupakua programu tumishi husika (Shake Flashlight & Camera) ifungue na utauona ujumbe utaojitokeza kuhusu matumizi ya betri kwenye programu tumishi hiyo. Unaweza kuchajua Cancel kwa maana ya kuupuzia kile kilichoelezwa au ukachagua “Don’t show again” na kubofya “Disable“.

tochi

Kitu cha kwanza kinachoonekana baada ya kufungua programu tumishi-Shake Flashlight & Camera ambapo unaweza kuchagua kubofya Cancel au Disable.

Hatua ya pili ni kuwasha kitufe (kupeleka upande wa kulia) kwa maana ya kuruhusu (on) kwenye kipengele cha tochi (Flashlight). Halikadhalika, utafanya hivyo hivyo iwapo utapenda pia kuwasha kamera kwa kuitikisha tu.

tochi

Jinsi ya kuwasha au kuzima kamera/tochi kwa kutikisha tu.

Ikitokea unapenda kuzima kipengele hicho kisifanya kazi tena au hutaki kuwa na programu tumishi kwenye simu yako basi unazima vipengele husika (weka off) kisha iondoe programu tumishi kama ambavyo huwa unaondoa nyingine.

Post a Comment

Previous Post Next Post